Tuesday, August 6, 2013

Ligi kuu UK

Kwa kuanzia na msimu mpya wa ligi kuu nchini Uingereze.Tutawaletea kila linarojiri kuwa teyari kupata yajayo.

Ahsante

Monday, March 12, 2012

Van Persie akubali offer ya Man City?

Manchester City wako tayari kumfanya Robin Van Persie kuwa mchezaji anayelipwa mshara mkubwa kuliko mchezaji yoyote kwenye ligi kuu ya Uingereza, ambapo atakua akipokea kiasi cha paundi 210,000 kwa wiki.

Mkataba huo unathamani ya paundi milioni 10.9 kwa mwaka, Chazo kimoja cha The Sunday Times kimeripoti kwamba kimsingi Van Persie amekubali dili hilo litalomuingizia kitita kikubwa cha pesa.

Bado timu zote mbili za Manchester City na Arsenal hazijafanya makubaliano rasmi, Ingawa Arsenal inaonekana kutaka kumzuia mshambuliaji huyo nyota aliyepiga mabao 32 katika michezo 37 aliyocheza msimu huu asiondoke klabuni hapo.

Van Persie 28 anatarajia kumaliza mkataba wake na Arsenal mwisho wa msimu ujao (mwezi wa sita 2013) na kocha wa Manchester city amekua akielezea ni kwa kiasi gani anamkubali mshambulijai huyo.

Mario Balotelli na Yaya Toure nusura wazichape kavukavu

Wachezaji wa Manchester City Mario Balotelli na Yaya Toure nusura wazichape kavukavu wakati timu zinaenda mapumziko kwenye mechi dhidi ya Swansea City kwenye mfululizo wa mechi za ligi kuu ya Uingereza hapo jana, Mechi hiyo iliisha kwa Manchester City kulala kwa bao moja bila majibu.

Chombo cha habari cha The Sun kilieleza kuwa utata huo ulizuka baada ya wachezaji hao wawili kuanza kurushiana maneno kwa sauti kali wakati wakielekea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.Iliwachukua muda kidogo wachezaji hao kurejea dimbani kuendelea na mchezo huo wakati kipindi cha pili kilipoanza.

Wakati wanaelekea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo Balotelli na Toure walionekana wakitetea jambo fulani kwa umakini wa hali ya juu. Lakini mambo yalibadilika walipoingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo na wakasikika wakikaripiana kwa hasira. Ingawa kocha wao Roberto Mancini alisema hajui lolote kuhusiana na suala hilo.

Alipoulizwa, kocha huyo raia wa Italia alisema “Hapana, sijui lolote kusiana na suala hilo.”

Suarez ajipendekeza mwenyewe PSG

Klabu ya Liverpool ya Uingereza imeshtushwa na taarifa za mshambuliaji wao wa Kutegemewa Luis Suarez kutamani kucheza pamoja na mchezaji mwenzake wa Urguay Diego Lugano anayekipiga kunako klabu ya PSG.

Suarez aliuambia mtandao wa 10 Sport kwamba “Ningependa kucheza klabu moja nae (Lugano). Ndio naweza kuja Paris.Kuna klabu nyingi zenye pesa ambazo zina

Manchester United kileleni

Wayne Rooney ameiweka Manchester United kileleni kwenye msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi moja baada ya kushinda mchezo wao wa Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya West Bromwich Albion 2-0 katika uwanja wa Old Trafford, matokeo ambayo yamepokewa kwa furaha zaidi na mashabiki wa United hasa baada ya mahasimu wao wakubwa na waliokuwa wakiongoza ligi, Manchester City kukubali kipigo cha 1-0 nyumbani kwa Swansea City.

Kwa matokeo hayo, United wamefikisha jumla ya pointi 67 huku City akibaki na pointi zake 66.

Mchezo mwingine ambao umeanza hivi punde unazikutanisha Norwich City wanaoikaribisha Wigan Athletic.

2011-2012 LIGI KUU YA BARCLAYS

Kwa ujumla
Nyumbani
Ugenini

Nafasi
Timu P W D L F A
W D L F A
W D L F A
GD Pts
1 Manchester United 28 21 4 3 68 27
11 1 2 39 15
10 3 1 29 12
41 67
2 Manchester City 28 21 3 4 69 20
14 0 0 42 6
7 3 4 27 14
49 66
3 Tottenham Hotspur 28 16 5 7 52 34
10 2 2 30 13
6 3 5 22 21
18 53
4 Arsenal 27 15 4 8 55 38
9 2 2 29 11
6 2 6 26 27
17 49


Saturday, March 10, 2012

Roberto Mancini amkasirisha Wenger

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amekasirishwa na kitendo cha Kocha wa Manchester City Roberto Mancini Kuongea hadharani kuelezea jinsi anavyomujhitaji Van Persie kwenye timu yake.

Gazeti la Uingereza London Evening Standard limesema kwamba Wenger amepatwa na hasira Kwa kitendo cha Mancini kumuongelea Mchezaji ambaye ana Mkataba na Timu mpaka mwaka 2013,Kwa sasa wenger Anapata wakati mgumu kuhakikisha Van Persie anaingia Mkataba mpya na Arsenal.

Van Persie Ameomba makubaliano juu Mkataba mpya yasogezwe mbele mpaka Mwisho wa msimu,Na inasemekana kumaliza Ndani ya nne bora kwenye ligi ya Uingereza ndicho kigezo kikubwa kitakachomfanya Van Persie Kubaki Arsenal.

Friday, March 9, 2012

van Persie amtia hofu Wenger

TIMU ya Arsenal imeingia katika hofu kubwa kutokana na hali ilivyo kwa mchezaji wake tegemeo, Robin van Persie ambaye juzi alishindwa kufanya mazoezi na timu yake ya taifa ya Uholanzi, kwa kile kilichoelezwa kusumbuliwa na maumivu.

Mchezaji huyo alishindwa kucheza katika dakika zote pale Uholanzi ilipocheza na England, hivyo kuanza kuwatia hofu mashabiki wa timu hiyo.

Kocha Arsene Wenger amesema kwamba, atafuatilia kwa karibu zaidi afya ya mchezaji huyo.