Tuesday, March 6, 2012

FREEMASONS IN TANZANIA


Kama unadhani kizazi hiki kinachoabudu ibada za Kabballah (wayahudi) na chenye kujiona ni zaidi ya binadamu wengine, kwamba ni kidogo utakuwa unajidanganya. Kama unadhani kizazi hiki kinatoa misaada kwa watoto yatima, na watoto waishio katika mazingira magumu unajidanganya.

Kama unadhani kutembelea tovuti yao yenye kujipambaunua kwamba inasaidi jamii kwa kiasi kikubwa, basi unajilimbikizia ujuha. Kama unadhani Freemasonry wapo Dar es salaam pekee basi uko nyuma yam shale wa saa unavyokwenda.

Iwapo ulidhani huna ndugu ambaye anaajira za Freemasonry basi unaweza kujidanganya pia huku ukijigamba kwamba unazo pesa za ‘kumwaga’. Na kama unadhani kuna mfanyabiashara nchini ambaye anatoa sana misaada kwa jamii kwamba inatokana na mavuno yake, basi unajidanganya.

Kama unaamini hutumii bidhaa za Freemasonry unajiongopea mwenyewe. Ni wakati wako wa kuchunguza kipi kipo wapi na nini kinaendelea nchini mwetu. Ziko pesa, badhaa na mabo lukika yenye nembo za Freemasons ambayo wewe unadhani ni muhimu katika maisha yako. Kifupi wametukamata.

Freemasons wasikudanganye kwamba wao ni imani za mwenyezi mungu ambaye amewatuma kuja kuwasaidia watu wenye dhiki. Kama ni hivyo basi tusingeliona utawala wa Marekani unakuwa wa Ki-Freemasons na kumaliza maisha ya Wairak, Wavietnam na kwingineko.

Na walivyo na sura za upole na kuchukuliwa kama watoa misaada kwa watu masikini, basi tumewapa tiketi ya kuziingilia nyumba zetu watakavyo. Ndiyo ni miaka 79 sasa kizazi hiki cha shetani kinachoruhusu wanaume pekee kuingia humo. Umejiuliza kwanini wanawake hawakubaliki? Tafakari.

Kwa taarifa yako kuna binadamu anaitwa Rockefeller anataka binadamu wote tuwekewe Microchip ili taarifa zetu zichukuliwe na satellite na kuziweka katika kompyuta moja. Wanataka kututawala kimwili sasa baada ya kufanikisha kututawala kiakili.

Rockefeller Mmarekani huyu ni adui namba moja wa binadamu walioumbwa na mwenyezi mungu. Katika azimio hilo ambalo kiambato chake ni New World Order kilichotangazwa n asana muumini wa Freemasons George Bush na ambaye nduguye Marvin Bush alipewa dhamana ya kulinda WTC kabla ya kulishambulia-kisha wakadanganya ni Osama Bin Laden.

Kama unadhani mfumo huu wa Microchip ni dhihaka, nakuachia kiungo hiki msomaji wangu mpendwa umfuatilie kiumbe huyu dhalimu; www.nexusmagazine.com/articles/rockefeller.html. ni kiumbe hatari kama ilivyokuwa kwa Adolf Hitler ambaye alikuwa kiumbe wao.

Ni hawahawa sasa wamejipa mamlaka ya kila kitu katika tawala mbalimbali ikiwemo Tanzania. Na wametushika kwa mambo mengi sana, mara utasiki misaada ya kiutu, mara leo utasikia Vicoba (kuna mkono wa Freemasonry hapo), na mengineyo.

Freemasons wapo nchini Tanzania kwa miaka 79 sasa, wakiendesha shughuli zao na kuwapumbaza watu. Wanafanya hila zao kwa kudai kuwa ni watumishi wa mungu tusiyemuamini. Wanajieleza kwa umakini sana ili kutolipua siri zao.

Soma maneno haya ambayo yalitamkwa na binadamu Sir Jayantilal Kashavji, ‘Once a Freemasons, always a Freemasons’. Inawezekana ikawa mgeni kwako, lakini ukitajiwa binadamu aitwaye Andy Chande siyo geni kwako. Nasadiki kwa dhati kabisa jina la pili limetoakana na kujiunga na Freemasonry.

Tunaambiwa ndani ya miaka 79 kipenzi chetu Mwalimu Nyerere alijua uwepo wao, lakini unaweza kujiuliza swali kwani imesemwa wakati yeye amekwisha kufariki? Na inaelezwa kuwa Mwalimu hakuwa Freemasonry(sijui angelikuwa hai angelisemaje).

Kwa maneno yao wenyewe wanajigamba kwa kusema ‘Freemasons is natural or Instictive fellowship between people of similar interest’. Inawezekana maneno haya yasiwe na maana kwako, lakini kuna swali jepesi moja tu. Je wanawake hawana ‘similar interest’ na Freemasonry (wanaume)?

Maneno yote ninayokupa ndugu msomaji sijatunga, na wala mimi siyo mtungaji wa makala hizi, bali mtafiti. Sitafiti kisha niandike bali nilikwisha kufanya hilo na ninaendelea ndiyo maana nakupa viungo kadhaa ujipe nafasi zaidi.

Mnamo April 3, 2005 Sir Jayantilal Kashavji au Andy Chande alifanya mahojiano na mwandishi mwandamizi Muhidin Michuzi. Msomaji mahojiano hayo yapo katika gazeti la Sunday News la April 3, 2005. Kuna maswali zaidi ya 100 ambayo ninaweza kuyauliza tokana na majibu ya mheshimiwa huyo.

Lakini swali langu la msingi ningelimwuliza kutokana na maneno yake haya; ‘I joined Freemasons 1954. However it took me two years to complete the process’. Kwamba licha ya kujiunga na Freemasons, ilimchukua miaka miwili kumaliza taratibu zote. ‘Taratibu’ zipi hizo iwapo ni jumuiya inayosadiki mungu?

Yaani nikiamua kujiunga na dini mojawapo sasa kati ya Ukristo au Uislamu toka Uafrika wangu, nichukue miaka miwili kumaliza ‘taratibu zote’? Ni taratibu gani mlizopewa enyi kizazi cha nyoka? Kizazi kilichovamia na kufanya mauaji huko Iraq na kuwaua wale wasiokuwa wanachama wao.

Sir Jayantalal Kashavji au J.K Chande au Andy Chande anatanabaisha kuwa kuwa Freemasons ni jumuiya iliyopo chini ya utawala wa United Grand Lodge ya Uingereza na Wales (soma Sunday News la April 3, 2005).

Hakukuwa na jipya sana katika majibu yake kwani inaonekana kulikuwa na ujuvi wa pande mbili kabla na baada ya mahojiano. Tunafahamu kuwa uzinduzi wa Freemasons ulifanyika chini ya utawala wa Rais Benjamini Mkapa, je kuna uhusiano gani kati ya kizazi hicho na uanzishwaji wa Bank M? funua akili yako!

Unaelewa ninachokuuliza na unagundua ninachomaanisha? Kwa maneno yake Andy Chande (Jayantalal Kashavji anawataja viongozi wanaowasapoti; Benjamini Mkapa (Tanzania), Moody Awory (Kenya), na Yoweri Museven (Uganda) kwa eneo la afrika mashariki.

Msomaji ukikumbuka makala mbili zilizopita ninataja sana serikali ya dunia. Na ukitazama uongozi wa J. K Chande unaunganisha Tanzania, Uganda, Shelisheli na Kenya, unaweza kupata jawabu kuwa hili ni jimbo, mtaa, kata ama kijiji cha Freemasons?

Na wengine sasa mnalia kuhusu suala la NICOL, basi unachopaswa kukifahamu kuwa kuna baadhi ya waandamizi wa kizazi cha Freemasonry hapo. Siyo jambo geni na wala halishangazi kwa wanazuoni. Tunajua ni akina nani walihudhuria sherehe ya uzinduzi. Na hata ile ya kutimiza miaka 75 ilipofanyika wakati wa awamu ya tatu.

Kwanini sherehe ya kutimiza miaka 75, mwaka 2005 ilitangazwa kuliko huko nyuma kwamba freemasonry wapo nchini au vinginevyo? Kwani ulikuwa wakati wa kutaja kuwa ni jumuiya isyofahamika kwa watu wakati ni jinsia moja tu inahiutajika?

Unaweza kupuuza sana suala hilo, na kama J.K Chande anavyosema kwa maneno yake mwenyewe haya; ‘Nyerere was not a Freemasons, but he knew what Freemasonry is’. Msomaji unaona ninachokiona hapo? Unaelewa ninachokielewa? Kwamba alifahamu, je ndiye aliyewasajili na kuingia nchini Tanzania?

District Grand Master Jayantalal Kashavji alituhabarisha kuwa ameongoza Freemasons kwa miaka 50 na ameamua kustaafu. Ukitaka kumfahamu bosi mpya wa Freemasons Tanzania nakuachia kiungo hiki; http;//www.ippmedia.com/guardian.2006/10/27/77236.html.

Na kwa wale wasomaji ambao hawana muda wa kutembelea mtandaoni, nakutaka usome gazeti la Guardian la tarehe 27/10/2006 (uk 4) habari iliripotiwa na Judica Tarimo. Hata hivyo wale wanaokubaliana nami, basi wafahamu kuwa bosi huyo ni Suryakant Ramji, msaidizi wake ni Tanna Sreekumar.

Na bosi wa eneo lote la afrika mashariki (yaani Tanzania, Uganda, Kenya na Shelisheli ni Dr Vilendra Talwar). Freemasonry wanawanachama zaidi ya milioni 5 hadi mwaka 2005, kizazi hiki cha nyoka kilianza mwaka karne ya 13. Na kwa Tanzania makao makuu yao ipo mitaa ya Sokoine (Sokoine Drive) mkabala hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam.

Vituko na ibada hizo za kishetani haziko Dar es salaam pekee, huko Arusha zimejazana na historia yake ni inajieleza wazi. Nitaeleza. Mnamo Julai 14, 2001 kulifanyika kikao cha Ki-freemasons Mount Meru Lodge.

Awali makao hayo yalipewa namba ya usajili 5363 kati ya mwaka 1932, lakini uanachama wake ulishamiri zaidi kulipoibuliwa vita ya pili ya dunia. Ndugu msomaji vita hiyo siyo kama tunavyodanganywa katika mashule yetu, kwani wenyewe wanaelewa ninachomaanisha hapa.

Huku vita hivyo vikiendelea, usajili wa ngome mpya za Freemasons ulikuwa ukifanywa. Na Arusha ilikwisha kupata namba ya awali (tazama hapo juu). Hivyo tangu mwaka 1957 Mount Meru Lodge ikapewa namba 7504. Ambapo kikao chao cha awali kilifanyika Kilimanjaro Lodge ya ki-freemasons No. 5111 mjini Moshi.

Kuna wamiliki wa Televisheni, na matajiri wakubwa ambao wanaabudu ibada za kishetani. Wanatumia utajiri huo kuwafumba watu kuwa wao wanasaidia jamii. Wanahadhi kubwa mbele ya watawala wetu, wanaheshimika mbele ya mawakala wa CIA (ambao ni mabalozi tulionao).

Wapo wanaounga mkono u-freemasons Tanzania huku wakiwa wanachama; Dr Edward Tenner (mgunduzi wa Vaccination), Dr William Mayo na Charles Mayo (waanzilishi wa kliniki ya moyo Marekani). Mwanzilishi wa tifa la Uturuki Jenerali Mustafa Kamal Atatuk, Mchungaji William Booth (mwanzilishi wa Salvation Army-jeshi la wokovu).

Wengine Padre Francisco Calvo (Padre wa kikatoliki aliyeanzisha Frremasonry huko Costa Rica mwaka 1865), Mchungaji Jesse Jackson (mwanzilishi wa Rainbow Coalition), Aga Khan (Kiongozi wa madhehebu ya Ismailia) 1877-1957. lakini swali linasalia kuhusu Aga Khan III(je ni mwendelezo wa freemasonry?).

Yupo Thomas Watson! Humfahamu huyu? Unaweza kuitazama kompyuta yako ndugu msomaji, kama imeandikwa IBM huyu ndiye mwanzilishi. Kuna J. Edgar Hoover (mkurugenzi wa FBI). Hapa nikuachie kiungo hiki msomaji; http;//calodges.org/no406.famasons.htm.

Usidanganyike kuwa kizazi hiki kinahubiri dini za mwenyezi mungu unazozijua, na wenyewe wanadai hakuna majadiliano kuhusu dini. Na msomaji aliyeuliza kuhusu Rais Obama, nitamwuliza; je unakumbuka kuwa tuliambiwa kiapo chake cha Urais kilikosewa hivyo wakarudia? Tafakari hilo, nipe jibu.